keep

vt,vi 1 weka, zuia; fanya kuwa ~ the class quiet nyamazisha darasa. ~ somebody indoors zuia mtu asitoke nje. ~ eye on (colloq) angalia kwa makini, linda. ~ something in mind kumbuka. 2 endeleza, weka ~ somebody waiting ngojesha, fanya mtu aendelee kungoja. ~ somebody going wezesha mtu kuendelea shs 10,000/= will ~ me going for four days shiiling 10,000/= zitanitosheleza kwa siku nne. 3 ~ somebody/something from doing something zuia, kinga you must ~ the wall from falling lazima uzuie ukuta usianguke we couldn't ~ from crying hatukuweza kujizuia kulia. 4 ~ something (back) (from) ficha I can't ~ anything (back) from you siwezi kukuficha kitu; zuia, kata the employer ~s back 3000/= a month for my pension mwajiri wangu hukata 3000/= kila mwezi kwa ajili ya kiinua mgongo changu. ~ something to oneself (often imper) hifadhi, dhibiti, kaa na (kitu) ~ your views to yourself usiseme/usitoe maoni yako; nyamaza. 5 (with an implied complement) timiza ~ a promise timiza ahadi ~ the law fuata sheria. 6 adhimisha ~ one's birthday adhimisha siku ya kuzaliwa. 7 linda. 8 hifadhi, tunza ~ the money for me nitunzie fedha zangu. ~ a firm/tight hold on shika imara. 9 ruzuku, kimu; fuga his salary ~s him and his family mshahara wake unamkimu yeye na familia yake he ~s cattle on his farm anafuga ng'ombe katika shamba lake. 10 weka ~ a note of something weka kumbukumbu ya kitu ~ a ledger tunza daftari. ~ accounts tunza mahesabu. 11 -wa na, miliki ~ a shop -wa na duka. shopkeeper n mwuza duka. 12 tunza, simamia. ~ a house tunza nyumba. ~ open house -wa tayari kukaribisha wageni/marafiki. 13 ~ on/to endelea. K~ cool (fig) tulia! poa! ~fit kaa imara/bora wa afya ~ to the left enda upande wa kushoto ~ straight on enda moja kwa moja ~ right enda upande wa kulia. 14 ~ (on) doing something endelea kufanya jambo, fanya jambo mara kwa mara ~ smiling endelea kutabasamu my shoe ~s (on) coming off kiatu changu kinatoka mara kwa mara. ~ going endelea bila kusimama/kukoma. 15 (of food) -toharibika, kaa the food will ~ till tomorrow evening chakula hakitaharibika/kitakaa hadi kesho jioni. 16 (uses with adverbial particles and preps) ~ at something shikilia; kazania; fanyia kazi, sikate tamaa. ~ somebody at something kazania mtu aendelee na jambo fulani, himiza, tia ari. ~ away (from) (something) epuka, kaa mbali na ~ away from the dog mwepuke yule mbwa. ~ somebody/something away (from) epusha, zuia asikaribie. ~ back (from something) kaa/baki nyuma. ~ somebody back zuia mtu asiende mbele. ~ somebody down gandamiza, dhulumu. ~ something down zuia ~ down your anger zuia hasira yako; punguza ~ down your expenses punguza matumizi yako. ~ in (eg of fire) endelea kuwaka the fire will ~ in till I come back moto utaendelea kuwaka mpaka nitakaporudi. ~ in with somebody endelea kuwa na uhusiano mzuri, elewana/patana. ~ somebody in zuia kama adhabu. ~ off kaa mbali. ~ off something -sikaribie kitu fulani, -tojihusisha na. ~ somebody/ something off zuia ~ your hands off me usiniguse. ~ on (doing something) endelea, shikilia. ~ on working endelea kufanya kazi. ~ something on endelea kuvaa. ~ somebody on endelea kumwajiri mtu. ~ on at somebody sumbua kwa malalamiko, maswali n.k. ~ out (of something) kaa mbali, -tojiingiza. ~ somebody/something out (of something) zuia kuingia ~ out of my business usingilie shughuli zangu. ~ to something timiza, fanya jambo lililokubaliwa ~ to your promise fanya kama ulivyoahidi, timiza ahadi yako. ~ to oneself jitenga, epuka kukutana na watu. ~ somebody/ something under tawala, zuia ~ the fire under zuia moto usienee. ~ up (with somebody) enda kwa kasi/ mwendo sawa na mtu mwingine Juma kept up with his classmates Juma aliendelea sawa na wenzake. ~ up with the Joneses shindana na majirani (katika kuhodhi vitu) (gari, nguo n.k.). ~ somebody up chelewesha mtu kulala mapema Don't ~ the children up usiwacheleweshe watoto kulala. ~ something up zuia kitu kisizame au kuteremka chini ~ up your courage jijasirishe zaidi; fuata, heshimu ~ up old customs endeleza/fuata mila za kale; endelea we will ~ up the discussion the whole day tutaendelea kujadili mchana kutwa; tunza it costs me a great deal to ~ up my farm inanigharimu sana kulitunza shamba langu. ~ it up endelea. n 1 riziki, chakula. 2 mnara wa ngome/boma. 3 for ~s (colloq) kwa kudumu, daima, abadani this is mine for ~s hii ni mali yangu kabisa/abadani. keeper n 1 mlinzi, mwangalizi. 2 (in compounds) gate ~er n bawabu. park ~er n mwangalizi wa hifadhi. keeping n 1 hifadhi, ulinzi. in safe ~ing mahali pa usalama. 2 (in verbal senses) ufugaji. in/out of ~ ing (with) -a kupatana/-siopatana na. keepsake n kumbukumbu, ukumbusho.